BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VVU TANZANIA (NACOPHA ) Limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Makamu Mwenyekiti wa Baraza Bi.Thereza Michael kilichotokea leo mchana katika hospitali ya mkoa alipolazwa kwa matibabu Mjini Musoma. 
Uongozi wa NACOPHA unatoa pole na kuungana na Familia ya Marehemu, Ndugu , Jamaa na Marafiki wote walioguswa na msiba huu, tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu awajalie uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.
Pumzika kwa Amani Ndugu yetu Mpendwa