Konga ya Wilaya ya Muleba imefanya uchaguzi, wa kuwachagua viongozi wapya baada ya viongozi wa awali kumaliza muhula wao wa kwanza.

Uchaguzi huo ulifanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Muleba ambapo uliratibiwa na kusimamiwa na Afisa wa Asasi na uimarishaji ubora Bwana Joseph Bukula wa shirika la JSI R& T kupitia mradi wa CHSSP Unaofadhiliwa na shirika la msaada kutoka kwa watu wa Marekani USAID, NACOPHA Kanda ya Mwanza na Ofisi ya maendeleo ya jamii chini ya Mratibu wa kudhibiti UKIMWI Halmashauri ya  Wilaya ya Muleba

Uchaguzi huo ulihudhuliwa wa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la watu wanaoshi na VVU bwana Deogratius Rutatwa, Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii, Mratibu wa UKIMWI wilaya upande wa tiba (DACC), Mratibu wa UKIMWI wilaya upande wa jamii (CHAC), Mratibu wa Kanda – NACOPHA/SAUTI YETU, Afisa tathmini na ufuatiliaji – NACOPHA/SAUTI YETU, Afisa wa asasi na uimarishaji ubora – JSI R&T/CHSSP, na wajumbe kutoka viikundi 25 vya WAVIU wilaya ya Muleba.





Viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni pamoja na:
Romward Nkororo – Mwenyekiti wa Konga
Malapia Athanasio – Makamu Mwenyekiti
Lameki Ndyamukama – Katibu wa Konga
Febronia Paskali – Mhasibu wa Konga

Viongozi wengine waliochaguliwa ni wajumbe wanne wa Konga, Uwakilishi wa Vijana pamoja na wajumbe wawili watakao wakilisha katika kamati ya kudhibiti UKIMWI ya Wilaya (CMAC)
Baraza kupitia Afisa Mtendaji Mkuu inatoa pongezi kwa viongozi waliochaguliwa na kuwataka watekeleze wajibu wao kufuatana na sheria ya baraza inavyowataka wafanye. Hivi sasa Baraza lina konga zipatazo 154. 

Baraza linatoa shukrani za dhati kwa JSI R&T kupitia mradi wa CHSSP kwa kufanya kazi kwa Karibu na Baraza kwa kuhakikisha malengo ya pamoja ya kufikia 90-90-90 yanafikiwa.