Wito huo umetolewa na Mratibu wa
TACAIDS Mkoa wa Mbeya Bwana EDWIN MWELEKA wakati wa ufunguzi wa warsha ya siku
mbili ya utambulisho na kuandaa mpango wa utekelezaji wa mradi wa SAUTI YETU
unaofadhiliwa na shirika la misaada ya maendeleo la kimataifa la Marekani
(USAID) na kutekelezwa Baraza la Taifa la watu wanaoishi na VVU (NACOPHA).
Warsha hiyo imefanyika Mkoani
Mbeya na Kujumuisha waratibu wa UKIMWI wa Halmashauri, Wenyeviti, Makatibu wa
konga wakiwakilisha konga ambao ndio
wanufaikaji wakuu na watekelezaji wa mradi wa SAUTI YETU kutoka katika
Halmashauri 16 pamoja na Waratibu wa
TACAIDS kutoka mkoa wa Njombe, Iringa na Mbeya.
Post a Comment