Tarehe 13/2/2017 kulifanyika kikao kati ya uongozi wa Konga temeke pamoja na ugeni kutoka UNAIDS. Mgeni toka UNAIDS Bi. Maria Engel mshauri mkuu wa miradi ya UNAIDS hapa nchini akifuatanana Afisa mipango wa NACOPHA ndg. Richard Muko, na Bi. Victoria Habuya ambaye ni afisa Ufuatiliaji na tathimini katika mradi wa SAUTI YETU.


Wageni hawa walikutana na wajumbe wa timu ya Uratibu na mawakili tiba wa konga ya Temeke kwa lengo la kutathmini jinsi konga za NACOPHA zitakavyoweza kutekeleza miradi ya kijamii ya kupambana na Saratani ya Shingo ya Kizazi. Pia wakakielezea kikao kwamba kutakuwa na mradi wa kupambana na shingo ya kizazi utakaofadhiliwa na shirika la Pink Ribbon Red Ribbon (PRRR)  utakao tekelezwa kwa ushirikiano kati ya NACOPHA na Tanzania Network of Women Living with HIV and AIDS (TNW+) katika maeneo ya Geita, Njombe, Tanga, Morogoro, Mara na Songwe.

Kama inavyofahamika hivi sasa saratani ya shingo ya kizazi ni ugonjwa unao enea kwa kasi sana hapa nchini. Wanawake waishio na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) wanaathirika kwa kiasi kikubwa kuliko wanawake wengine, hivyo kuna uhitaji wa kuibua mikakati ya kuwalenga kwa karibu. Majadiliano yalihusu ni jinsi gani WAVIU wanaweza pia nao kuhusika katika mapambano hayo katika konga za NACOPHA. Kwa kuwatumia mawakili tiba, timu ya utekelezaji za Konga kata wakiungana na timu ya uratibu ya Konga kwa pamoja ili kuwe na mikakati ya kuwasaidia wanawake WAVIU kuzuia maambukizi ya saratani ya shingo la kizazi.

Baada ya majadiliano wajumbe walikubaliana kuwa njia pekee ni kutoa elimu sahihi juu ya Saratani ya shingo ya kizazi, kampeni ya upimaji wa mara kwa mara kwa WAVIU na kuunda timu itakayopewa mafuzo ili nao waweze kuendeleza elimu hii kwa WAVIU wengine (TOT).


Ili miradi kama hii iweze kufikia walengwa inabidi mikutano na viongozi wa Serikali ya mtaa iandaliwe, pawe na kampeni za matangazo pia pawe na vipeperushi katika kuhamasisha watu kupima. Aidha tulikubaliana muda wa upimaji katika vituo vya afya kila siku uongezeke na uwe endelevu kwa watu wote mchanganyiko.

Story na BAITAN JAPHEES. Katibu Mkuu Konga Temeke