·         Katika kuadhimisha miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania, Baraza la watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Tanzania (NACOPHA) linampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Joseph Pombe Magufuli pamoja na Serikali yake katika kuendeleza jitihada za kudumisha  Hekima, Umoja na Amani tulioachiwa na Muasisi wetu Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

·         NACOPHA ina tambua jitihada zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano chini ya  Mhe. Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli katika shughuli za mwitikio wa UKIMWI kwa lengo la kufikia mkakati wa kimataifa wa kuhakikisha azma ya kufikia sifuri tatu yaani: Sifuri maambukizi mapya ya VVU, Sifuri Vifo vitokanavyo na UKIMWI pamoja na Sifuri unyanyapaa na ubaguzi.

·         NACOPHA inaendeleza jitihada zake katika kupambana na Virusi vya UKIMWI pamoja na Ubaguzi na Unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI na kuhakikisha kuna uimarishwaji , udhibiti na ugawaji dawa za ARV,kuhamasisha upimaji wa Virusi vya Ukimwi, kutokomeza maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Kuhamasisha elimu ya jinsia, Kutoa elimu ya afya ya uzazi kuboresha upatikanaji kondom za kike, utoaji damu salama kulingana na vigezo vya shirika la afya duniani. Kuendelea kuelimisha njia za kujikinga na maambukizo pamoja na kutoa elimu kuhusu mila na tabia hatarishi zinazochangia ongezeko la maambukizo.
·         Tunaimani, Upendo na Matumaini kwa taifa letu la Tanzania, sote ni Watanzania na bila kubagua hali zetu za maambukizo tunamchango mkubwa katika maendeleo ya nchi yetu ya Tanzania.


·         Tanzania bila UKIMWI Inawezekana.