Kila
tarehe 8 machi ya kila mwaka Tanzania huungana na nchi nyingine wanachama wa
Umoja wa Mataifa kuadhimisha siku ya wanawake Duniani.
Baraza
la Taifa la Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (NACOPHA) linaungana na Wanawake
wote Tanzania na Dunia kwa ujumla katika kuadhimisha siku hii muhimu ya Wanawake
duniani ili kuendeleza Utetezi wa Haki za wanawake na Usawa wa kijinsia,
ifikapo 2030 kuwe na asilimia 50 kwa 50 ya ushiriki wa wanawake na wasichana
katika Nyanja zote za maendeleo.
Katika
Kufikia Malengo hayo NACOPHA inatoa wito kwa Wanawake wote Tanzania Kuongeza Jitihada
siyo tu katika kufikia malengo ya 50 kwa 50 ifikapo 2030 bali pia kufikia
malengo yaliyowekwa kimataifa 90% 90% 90% ya Mkakati wa Kupunguza maambukizi ya
VVU ifikapo 2020 yaani:-
90%
kwa waliopima afya zao na kutambua hali yao ya maambukizi,
90%
wanaostahili kupatiwa tiba wanapata tiba na kubakia katika tiba na
90% ya waliopo kwenye tiba wawe na kiwango
kidogo cha virusi kwenye damu
Lengo likiwa ni kufuta kabisa UKIMWI ifikapo
mwaka 2030.
Rai yetu kwa Wanawake
wote: sasa ni wakati muafaka kujitokeza kwa wingi katika mwitikio wa UKIMWI ili
kudhibiti ongezeko la maambukizo ya VVU na kuhakikisha tunafikia sifuri tatu
ifikapo mwaka 2030.
Tunawatakia
Mafanikio mema katika kuadhimisha siku ya Wanawake duniani.
Post a Comment