Kamati ya Bunge ya UKIMWI na madawa ya kulevya ilikutana na Baraza la
Taifa la Watu Wanaoishi na VVU (NACOPHA) jijini Dar es Salaam na kujadili mambo
mbalimbali ikiwemo kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Baraza na kamati hiyo
kwa lengo la kuwasaidia watu wanaoishi na VVU kupata huduma bora za afya na
kuishi maisha bora
Kamati ya Bunge ililipongeza baraza kwa kazi kubwa Zinazofanywa kupitia
viongozi wake kutokana na mafanikio yalioainishwa, Pamoja na hayo kamati ya
Bunge imeahidi kushughulikia changamoto zilizoanishwa na Baraza ikiwemo suala
la kuhakikisha Baraza linapata ofisi ya kudumu, pamoja na Viongozi wa Konga
kupatiwa ofisi katika kila Halmashauri.
Mbunge kutoka Nsimbo katavi Mheshimiwa Richard Mbogo
ambae ni mjumbe wa kamati ya Bunge- alisema “ Sisi kama kamati ya Bunge tutakaa
na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI kupitia kamati za UKIMWI za Halmashauri na
kuwashauri kuwapatia viongozi wa Konga ofisi katika kila Halmashauri, ili
waweze kufanya kazi kwa ukaribu zaidi na Halmashauri katika mwitikio wa UKIMWI”.
Kuhusu ofisi ya makao makuu ya Baraza kamati hiyo iliahidi kukaa na shirika
la Taifa la nyumba na kuona ni kwa namna gani wanaweza kulipatia Baraza sehemu
kwa ajili ya ofisi ili kuliwezesha kufanya shughuli zake kwa ufanisi zaidi.
Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo Mheshimiwa Nasari Yahaya Omari
alilihakikishia Baraza kuwa kamati itatoa ushirikiano wa karibu pale
unapohitajika ikiwemo katika kutatua changamoto mbalimbali, pia aliahidi kukaa na
Serikali pamoja na mifuko ya Bima ya afya na kutazama vikwazo vinavyopelekea
kutopatikana kwa huduma za bima ya afya
kwa watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU).
Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Baraza Bwana Deogratius Rutatwa
ameishukuru kamati ya Bunge kwa kujitolea kufikisha matakwa ya Baraza kwa
TAMISEMI ikiwemo kuishauri kufanya kazi kwa ukaribu na Konga.
Aidha ameiomba kamati kuishauri TAMISEMI kutengeneza waraka utakaoonyesha
Halmashauri inatakiwa kufanya kazi na WAVIU
Katika hatua nyingine Bwana Rutatwa alimefurahishwa na kitendo cha kamati
hiyo kutoa fursa ya kuwatumia WAVIU katika shughuli za mwitikio wa UKIMWI na
katika matamasha makubwa ili kuihamasisha jamii juu ya maswala ya UKIMWI
Post a Comment