Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa nchini, Alvaro Rodriguez alipowasili katika viwanja vya Jamhuri jijini Dodoma katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya ukimwi duniani leo tarehe 01 Desemba 2018. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenyeulemavu.


Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Profesa Davis Mwamfupe alipowasili katika viwanja vya Jamhuri jijini Dodoma katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya ukimwi duniani leo tarehe 01 Desemba 2018. Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Profesa Faustine Kamuzora.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akikagua baadhi ya mabanda yaliyokuwa yakionyesha shughuli mbalmbali zinazoendeshwa na wadau alipotembelea mabanda hayo wakati wa hafla ya maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani leo tarehe 01 Desemba 2018 jijini Dodoma..


Baadhi ya waandamanaji toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora wakipita katiika maandamano wakati wa hafla ya siku ya ukimwi duniani leo tarehe 01 Desemba 2018 jijini Dodoma.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza wakati wa hafla ya maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani leo tarehe 01, Desemba 2018 jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu Mhe. Jenista Mhagama, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wezee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Dkt. Leornard Maboko.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza wakati wa hafla ya maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani leo tarehe 01, Desemba 2018 jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Binilith Mahenge, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wezee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Dkt. Leornard Maboko.


Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Dkt. Leornard Maboko akizungumza wakati wa hafla ya maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani leo tarehe 01, Desemba 2018 jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu Mhe. Jenista Mhagama na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wezee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile.


Mwenyekiti wa Baraza la Watu Wanaosihi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (NACOPHA), Bi. Leticia Mourice akizungumza wakati wa hafla ya maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani leo tarehe 01, Desemba 2018 jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu Mhe. Jenista Mhagama na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wezee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Dkt. Leornard Maboko.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akikata utepe kuzindua Mkakati wa Nne wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI 2018/19 - 2022/23 leo tarehe 01 Desmba 2018 jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Dkt. Leornard Maboko, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu Mhe. Jenista Mhagama,  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wezee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano, Mussa Sima. Mkakati huo unatarajia kupunguza maambukizi mapya ya VVU kwa asilimia 75 ifikapo mwaka 2020 na asilimia 85 ifikapo mwaka 2023.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimkabidhi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Seleman Jaffo nakala ya Mkakati wa Nne wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI 2018/19 - 2022/23 leo tarehe 01 Desmba 2018 jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Jenista Mhagama,  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wezee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano, Mussa Sima na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo. Mkakati huo unatarajia kupunguza maambukizi mapya ya VVU kwa asilimia 75 ifikapo mwaka 2020 na asilimia 85 ifikapo mwaka 2023.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimkabidhi Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa nchini, Alvaro Rodriguez nakala ya Mkakati wa Nne wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI 2018/19 - 2022/23 leo tarehe 01 Desmba 2018 jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Muwakilishi  Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia UKIMWI   Duniani (UNAIDS) Dkt. Leo  Zekeng, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Dkt. Leornard Maboko, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Jenista Mhagama na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wezee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile. Mkakati huo unatarajia kupunguza maambukizi mapya ya VVU kwa asilimia 75 ifikapo mwaka 2020 na asilimia 85 ifikapo mwaka 2023.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa masuala ya Ukimwi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani iliyofanyika kitaifa jijini Dodoma leo. (Picha zote na: Frank Shija - MAELEZO, Dodoma)