Baraza la watu wanaoishi na VVU (NACOPHA) mnamo Tarehe 22/7/2017 tulikuwa na uchaguzi wa viongozi katika Konga mpya ya Ubungo, uchaguzi huo ulifanyika katika ofisi ya manispaa ya Ubungo, ambapo wajumbe 39 kutoka katika vikundi vya WAVIU na Mitandao ya WAVIU, vilivyopo katika kata za wilaya ya ubungo, Mratibu wa UKIMWI wa Manispaa, Afisa Maendeleo ya Jamii na Vijana, Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa, Mwenyekiti wa kamati ya UKIMWI halmashauri ya manispaa ya Ubungo, Makatibu kutoka Konga za Temeke na Ilala, Mwenyekiti konga ya Kinondoni, Mwakilishi kutoka mfuko wa kudhibiti UKIMWI  (ATF), Ofisi ya NACOPHA Kanda ya Dar es Salaam, na Mratibu wa kanda toka JSI.


Uchaguzi huu uliratibiwa na kufadhiliwa na Shirika la JSI kupitia mradi wa CHSSP unaofadhiliwa na USAID. Katika uchaguzi huo uliochukua takriban masaa nane ulifanikiwa na viongozi wafuatao waliweza kuchaguliwa:-


1. Kyara Lweno- Mwenyekiti
2.Reinfrida Chitokota- Makamu Mwenyekiti
3. Jacqueline Alois- Katibu
4.Juliana P. Jaribu- Mweka hazina
5.Salum Kondo- Mjumbe mwakilishi wa Wanaume
6.Enos Tossye- Mjumbe mwakilishi wa Wanaume
7.Neema Duma- Mjumbe mwakilishi wa Wanawake
8.Salama Ally- Mjumbe mwakilishi wa Wanawake
9.Lucian Elias - Mjumbe mwakilishi wa Vijana wa Kiume
10. Anna Sajilo- Mjumbe mwakilishi wa Vijana wa Kike



Wawakilishi katika kamati ya UKIMWI ya Manispaa (CMAC)
1. Rogers Kaitila (Mwanaume)
2 .Mary Kuzenza (Mwanamke)


NACOPHA inatoa pongezi kwa viongozi hao waliochaguliwa na kuwataka watekeleze wajibu wao kufuatana na sheria ya baraza inavyowataka wafanye. Hivi sasa Baraza lina konga zipatazo 154. Baraza linatowa shukrani kwa JSI kupitia mradi wa CHSSP kwa kufanya kazi kwa Karibu na Baraza kwa kuhakikisha malengo ya pamoja ya kufikia 90%,90%,90% yanafikiwa. Bira kusahau Serikali kupitia kwa viongozi wa wilaya, CHAC na DAC tunawashukuru sana, TACAIDS na wadau wote waliosaidia kufanikisha kwa uchaguzi huo katika konga mpya ya Ubungo.










Mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI ni mapambano endelevu, kila mmoja kwa nafasi yake hana budi kuhakikisha kuwa anapigana kwa nguvu zote kuhakikisha tunatokomeza janga hili la UKIMWI.